MH. MAVUNDE KUCHANGIA GHARAMA ZA USAJIRI WA VIKUNDI 10 VYA SANAA KUPITIA TAMASHA LA DODOMA MPYA
8:08:00 PM
1 comments
Naibu Waziri, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Mheshimiwa Anthony Peter Mavunde ameahidi kulipia gharama za kusajiri Vikundi 10 chini ya Baraza la Sanaa la Taifa BASATA ikiwa ni sehemu ya kusaidia Kurasimisha kazi za Sanaa nchini. Mheshimiwa Mavunde ametoa ahadi hiyo akiwa Ofisini kwake Mkoani Dodoma baada ya Kutembelea na Mkurugenzi wa Kampuni ya Millennium Stars Entertainment ndg. Josias Charles ambaye alifika Ofisini kwa Mh. Mavunde kuzungumza nae juu ya Umuhimu wa Tamasha la Dodoma Mpya linalotarajia kufanyika kuanzia Tarehe 5/08/2017 na kuzunguka wilaya zote 7 za Dodoma huku hitimisho likifanyika katika uwanja wa Jamhuri Stadium kama taarifa zitakavyotolewa hapo baadae.
Josias Charles (Mkurugenzi wa Kampuni ya Millennium Stars Entertainment Company Ltd |
Itakuwa vyema sana
ReplyDelete